Taarifa hiyo imetolewa baada ya Shirika la Afya Duniani kutaka China kutoa maelezo na kuruhusu uchunguzi kufanyika kuhusu kilichosababisha mlipuko wa virusi vya Corona.
Maambukizi ya kwanza ya virusi vya Corona yaliripotiwa China, miaka mitano iliyopita.
Msemaji wa wizara ya Mambo ya Nje ya China Mao Ning amesema katika kikao na waandishi wa habari kwamba China iko tayari kushirikiana na kila mshirika katika utafiti wa kisayansi kote duniani na kutoa mchango muhimu katika kuzuia mlipuko wa magonjwa hatari katika siku zijazo.
Forum