Upatikanaji viungo

Breaking News
Jumatatu, Septemba 16, 2024 Local time: 22:25

Chama cha MK chataka uchaguzi Afrika Kusini urudiwe


Chama cha tatu kwa ukubwa cha kisiasa nchini Afrika Kusini kimeiomba mahakama kuu ya taifa hilo kuzuia kuanza baadaye wiki hii kwa bunge jipya, kikisema uchaguzi wa Mei 29 ulikumbwa na udanganyifu.

Bunge la Kitaifa limepangwa kuanza Ijumaa ili wabunge waapishwena kumchagua spika mpya, naibu wake na rais.

Hata hivyo, chama cha Umkhonto weSizwe (MK), ambacho kilishika nafasi ya tatu katika uchaguzi wa hivi karibuni, kimewasilisha malalamiko kisheria kuomba mahakama ya kikatiba ya Afrika Kusini kufuta uamuzi wa tume ya uchaguzi wa kutangaza uchaguzi ulikuwa huru na wa haki.

MK, ambacho kinaongozwa na Rais wa zamani wa Afrika Kusini, Jacob Zuma, kinadai kwamba kulikuwa na dosari katika upigaji kura na kuomba uchaguzi urudiwe.

Forum

XS
SM
MD
LG