Upatikanaji viungo

Breaking News
Alhamisi, Septemba 12, 2024 Local time: 21:06

Bunge la Iran halina imani na mawaziri wa rais mpya


Bunge la Iran, limepiga kura ya kutokuwa na imani kwa mawaziri waliopendekezwa na Rais Masoud Pezeshkian, ili kuanzisha rasmi serikali yake katika utawala wa 14.

Pezeshkian hapo awali alisema amepata idhini kutoka kwa ngazi za juu zaidi za mfumo wa nchi kwa wateule wake wote.

Pezeshkian aliingia madarakani baada ya kushinda uchaguzi wa ghafla mwezi uliopita, kufuatia kifo cha Rais Ebrahim Raisi mwenye msimamo mkali katika ajali ya helikopta mwezi Mei.

Kabla ya kura ya bunge Jumatano, Pezeshkian alisisitiza bungeni kuwatetea mawaziri waliopendekezwa na kusisitiza kwamba uteuzi wao ulipata kibali kutoka kwa kiongozi mkuu wa nchi.

Alisema kuwa awamu ya 14 imejitolea kutekeleza na kufuata sera za jumla za mfumo kama ilivyoainishwa na kiongozi mkuu Ali Khamenei.

Forum

XS
SM
MD
LG