Upatikanaji viungo

Breaking News
Jumamosi, Julai 06, 2024 Local time: 11:03

Baraza jipya la mawaziri limeapishwa Misri


Rais wa Misri Abdel Fattah al-sisi May 30 2024
Rais wa Misri Abdel Fattah al-sisi May 30 2024

Rais wa Misri Abdel Fattah al-Sisi, amewaazpisha mawaziri ambao alifanya mabadiliko ya baraza hilo, ikijumuisha uteuzi wa mawaziri wapya wa fedha na mambo ya nje.

Mabadiliko hayo yanajiri wakati Misri inakabiliwa na changamoto kadhaa ikiwemo vita vya Gaza kwenye mpaka wake, matatizo ya uchumi na ukosefu wa umeme.

Wakati baraza la mawaziri la awali lilopojiuzulu mwezi mmoja uliopita, Sisi alimteua tena waziri mkuu Mostafa Madbouly na kusema kwamba serikali yake mpya inastahili kuangazia namna ya kupunguza mfumuko wa bei na kudhibiti masoko pamoja na kuimarisha uwekezaji.

Ahmed Kouchouk ameapishwa kuwa waziri wa fedha. Alikuwa naibu wa waziri wa fedha. Anakabiliwa na changamoto kubwa sana ikiwemo uchumi unaodorora na mzigo mkubwa wa deni la serikali ambalo limekuwa likiongezeka katika miaka ya hivi karibuni.

Mawaziri wa Misri wana mamlaka madogo ya kufanya maamuzi. Nguvu zipo mikononi mwa rais, jeshi na huduma ya usalama.

Forum

XS
SM
MD
LG