Upatikanaji viungo

Breaking News
Jumapili, Machi 30, 2025 Local time: 15:21

Apigwa risasi na Walinzi wa White House


Mtu mwenye silaha anayeaminika alisafiri kutoka Indiana alipigwa risasi na maafisa wa Idara ya Ulinzi wa Viongozi ya Marekani, “U.S. Secret Service,” karibu na White House baada ya makabiliano mapema Jumapili, kulingana na mamlaka.

Hakuna mtu mwingine aliyejeruhiwa katika ufyatuaji risasi huo uliotokea usiku wa manane karibu na mtaa kutoka White House, kwa mujibu wa taarifa ya Secret Service.

Rais Donald Trump alikuwa Florida wakati ufyatuaji risasi huo unatokea. Idara hiyo ilipokea taarifa kutoka kwa polisi wa eneo hilo kuhusu madai ya “mtu aliyejiua” ambaye alisafiri kutoka Indiana na walikuta gari la mtu huyo ambalo linalo shabihiana na maelezo yaliyotolewa eneo la karibu.

“Maafisa walipomkaribia, mtu huyo alifyatua bunduki na makabiliano ya silaha yakatokea, ambapo risasi zilifyatuliwa na wafanyakazi wetu,” Idara ya “Secret Service,” imesema katika taarifa.

Forum

XS
SM
MD
LG