Upatikanaji viungo

Breaking News
Jumatatu, Aprili 21, 2025 Local time: 19:33

Afrika Kusini kuhalalisha biashara ya ngono


Rais wa Afrika Kusini Cyril Ramaphosa
Rais wa Afrika Kusini Cyril Ramaphosa

Afrika Kusini leo Ijumaa imesema haitaharamisha tena biashara ya ngono, ikitumai kukabiliana na viwango vya juu vya uhalifu dhidi ya wanawake katika nchi hiyo yenye idadi kubwa zaidi ya visa vya ukimwi duniani.

Uuzaji na ununuzi wa huduma za ngono hautachukuliwa tena kama uhalifu chini ya sheria iliyopendekezwa na wizara ya sheria.

Kulingana na makundi yanayotetea sheria hiyo, kuna zaidi ya wafanyabiashara wa ngono 150,000 nchini humo.

Waziri wa sheria Ronald Lamola ameuambia mkutano wa waandishi wa habari “Inatarajiwa kuwa kuhalalisha biashara hiyo kutapunguza ukiukaji wa haki za binadamu dhidi ya wafanyabiashara wa ngono.”

Afrika Kusini ni moja ya nchi yenye visa vingi vya ukimwi duniani na imekumbwa na ongezeko la wimbi la ukatili dhidi ya wanawake.

XS
SM
MD
LG