Taarifa kutoka ikulu ya Afrika Kusini inaeleza kwamba imepokea uamuzi wa marekani kujiondoa kutoka mpango huo wa JETP, kufuatia amri ya utendaji iliyotiwa saini na Rais Donald Trump.
Afrika Kusini ambayo inategemea zaidi mkaa kwa ajili ya kuzalisha umeme ilijiunga na JETP 2021 kwa lengo la kupata msaada wa kupunguza matumizi ya mkaa na kugeukia matumizi ya nishati safi mbadala.
Marekani iliahidi kutoa dola milioni 56 kwa mpango huo na kuongeza dola bilioni 1 kwa ajili ya uwekezaji wa kibiashara.
Nchi nyengine zinazopokea msaada kutokana na mpango huo ni Senegal, Vietnam na Indonesia.
Forum