Upatikanaji viungo

Breaking News
Jumamosi, Mei 18, 2024 Local time: 06:52

Uganda kuikopa benki ya China dola milioni 150 baada ya Benki ya Dunia kusitisha ufadhili


CRais wa Uganda Yoweri Museveni akipeana mkono na Rais wa China Xi Jinping huko Beijing. Picha na REUTERS
CRais wa Uganda Yoweri Museveni akipeana mkono na Rais wa China Xi Jinping huko Beijing. Picha na REUTERS

Uganda inalenga kukopa dola milioni 150 kutoka Benki ya China (Exim) kuimarisha miundo mbinu yake ya mitandao , wizara ya fedha ya nchi hiyo imetangaza.

Hatua hiyo inadhihirisha kuimarika kwa taifa hilo la Afrika Mashariki katika kutegemea mikopo ya China baada ya Benki ya Dunia kusitisha misaada yake kwa nchi hiyo kutokana na sheria kali dhidi ya wapenzi wa jinsia moja.

Wizara ya Fedha na wizara ya habari waliiomba Bunge kuidhinisha serikali kuomba mkopo huo kutoka Uchina.

Kulingana na wizara ya fedha, fedha hizo zitatumika katika kufadhili miradi ya serikali, uwekaji, uagizaji na usaidizi wa miundombinu ya kitaifa.

Aidha Uganda iko kwenye mazungumzo na wakala wa mikopo wa mauzo ya nje wa China SINOSURE na Benki ya Exim kwa mkopo wa kufadhili ujenzi wa bomba la kusaidia Uganda kuuza nje mafuta yake ghafi katika masoko ya kimataifa.

Benki ya Dunia, ambayo kwa kawaida ni mkopeshaji mkuu wa maendeleo wa Uganda, ilisitisha mikopo kwa Uganda baada ya Rais Yoweri Museveni kutia saini Sheria ya Kupinga Mapenzi ya jinsia moja ambayo inatoa hukumu kali ikiwa ni pamoja na kifo.

Forum

XS
SM
MD
LG