Uturuki haitafanya tena biashara na Israel yenye thamani ya dola bilioni 7 kwa mwaka hadi litakapopatikana sitisho la mapigano la kudumu huko Gaza na kuruhusu misaada ya kibinadamu kuwafikia Wapaletina bila ya kizuizi, waziri wa biashara wa Uturuki amesema leo Ijumaa.
Wanajeshi wa Russia wameingia kambi ya jeshi la anga nchini Niger ambayo ilikuwa inatumiwa na wanajeshi wa Marekani, afisa mkuu wa jeshi la Marekani ameliambia shirika la habari la Reuters, hatua inayofuatia uamuzi wa utawala wa kijeshi wa Niger kuwafukuza wanajeshi wa Marekani.
Idadi ya vifo kutokana na mafuriko nchini Kenya imevuka 200 tangu mwezi Machi, wizara ya mambo ya ndani imesema Ijumaa, huku kimbunga kikielekea pwani ya Tanzania.
Jimbo la Florida, Marekani, limepitisha sheria mpya inayopiga marufuku utoaji mimba baada ya wiki sita za ujauzito.
Mgombea anayaetarajiwa kuwa mteule wa urais wa kupitia chama cha Republican Donald Trump anasema akichaguliwa atarejesha tena marufuku ya kusafiri kwa baadhi ya nchi zenye waislamu wengi katika siku ya kwanza ya utawala wake mpya.
Rais wa Liberia Joseph Boakai siku ya Alhamisi alitia saini amri ya kiutendaji ya kuanzisha mahakama ya uhalifu wa kivita yenye lengo la kuleta haki kwa waathiriwa wa dhuluma kubwa zilizofanywa wakati wa vita viwili vya wenyewe kwa wenyewe katika nchi hiyo ya Afrika Magharibi.
Njaa na Utapiamlo unaenea kote nchini Sudan, mwaka moja tangu kuzuka kwa vita kati ya jeshi la Sudan na Kikosi cha dharura cha (RSF) huku ikiwa hakuna dalili ya vita kusitishwa hivi karibuni.
Jeshi la Marekani linapanga kurejea Chad ndani ya mwezi mmoja kwa ajili ya mazungumzo kuhusu kurekebisha makubaliano ambayo yanairuhusu kubakisha wanajeshi huko, jenerali mmoja wa Marekani alisema Jumatano.
Wabunge wa Marekani watapiga kura wiki ijayo, itakayobaini iwapo Spika wa baraza la wawakilishi Mike Johnson atasalia mamlakani, kwenye mojawapo ya nyadhifa za juu za uongozi katika serikali ya Marekani.
Hatua iliyoshangaza wengi ya kutangazwa kwa waziri mkuu mpya wa Haiti Jumanne, sasa inaligawanya baraza la mpito, lililoundwa hivi karibuni na kupewa jukumu la kuchagua viongozi wapya wa nchi hiyo ya Caribbean, yenye matatizo kutokana na uhalifu wa magenge.
Maelfu ya wafanyakazi duniani wameshiriki katika sherehe mbali mbali za kuadhimisha siku ya wafanyakazi ya Mei Mosi, wakidai nyongeza za mishahara na nafasi bora za ajira kutokana na kupanda kwa bei za chakula na mafuta.
Rwanda yaweka mkakati mpya wa ajira kwa vijana unaoambatana na mwelekeo wa dunia wenye mfumo wa teknologia katika kutoa huduma mbalimbali.
Pandisha zaidi