Watu wenye silaha wamewaua watu sita Nigeria.

Rais wa Nigeria Muhammadu Buhari.

Watu wenye silaha wamewaua watu sita, wakiwemo wahindi wawili, katika jimbo la Kogi nchini Nigeria, polisi walisema Jumamosi, huku eneo hilo likikumbwa na ghasia za wanajihadi na magenge.

Watu wenye silaha wamewaua watu sita, wakiwemo W]wahindi wawili, katika jimbo la Kogi nchini Nigeria, polisi walisema Jumamosi, huku eneo hilo likikumbwa na ghasia za wanajihadi na magenge.

Washambuliaji walilifyatulia risasi basi katika mji wa viwanda wa Ajaokuta Ijumaa usiku na kuwaua wahindi wawili, polisi wawili wasindikizaji na madereva wawili, msemaji wa polisi wa jimbo hilo William Ovye Aya alisema katika taarifa.

Wafanyakazi wawili wataalam kutoka nje, madereva wawili wa kampuni na inspekta wawili wa polisi walikufa katika majibizano ya risasi , Aya alisema.