Utawala wa Biden ulitangaza hatua ya mwisho ya utoaji msaada kwa Ukraine

Rais wa Marekani, Joe Biden katika picha iliyochukuliwa December 20, 2023.

Mfuko huo wa dola milioni 250 unajumuisha silaha za ulinzi wa anga, risasi za ziada za mifumo ya roketi ya hali ya juu (HIMARS)

Utawala wa Biden ulitangaza Jumatano kuwa hatua ya mwisho ya utoaji silaha na vifaa vya kijeshi kwa Ukraine kutoka kwa hifadhi za Marekani kwa mujibu wa idhini ya rais iliyopo, kwa misaada ya baadaye kwa Kyiv iko mikononi mwa Bunge.

Mfuko huo wa dola milioni 250 unajumuisha silaha za ulinzi wa anga, risasi za ziada za mifumo ya roketi ya hali ya juu (HIMARS), risasi za milimita 155 na risasi za milimita 105, na vifaa vya kukinga silaha, Waziri wa mambo ya nje wa Marekani, Antony Blinken alisema katika taarifa.

Msaada wetu umekuwa muhimu katika kusaidia washirika wetu wa Ukraine wakati wanaitetea nchi yao na uhuru wao dhidi ya uchokozi wa Russia, Blinken alisema akiongeza kuwa silaha na vifaa vilikuwa vinatolewa chini ya vikwazo vilivyoelezewa hapo awali kwa Ukraine.

John Kirby, msemaji wa Baraza la Taifa la Usalama akiwa mjini Washington

Wakati huo huo, msemaji wa Baraza la Taifa la Usalama John Kirby alisema wiki iliyopita kwamba Rais Joe Biden alipanga mfuko mmoja zaidi wa msaada wa kijeshi mwezi Desemba, lakini msaada huo baada ya hapo utahitaji makubaliano katika Bunge, ambapo matarajio ya makubaliano hayana uhakika.