Umoja wa Mataifa waonya huhusu ukosefu wa usalama wa chakula Niger

Mwanamke akitayarisha chakula mjini Niamey wakati UN ikionya kuhusu ujosefu wa chakula , Niger.

Umoja wa Mataifa Jumatano umeonya kuwa mzozo wa kisiasa unaoendelea Niger huenda ukaongeza ukosefu wa usalama wa chakula kwenye taifa hilo masikini, ukiomba kuondolewa kwa vikwazo na kufungwa kwa mipaka ili kuruhusu upelekaji wa misaada ya kibinadamu.

Shirika la masuala ya kibinadamu la Umoja huo, OCHA, limesema kwamba hata kabla ya rais wa taifa hilo aliyechaguliwa kidemokrasia Mohamed Bazoum kuondolewa madarakani, tayari taifa hilo lilikuwa na zaidi ya watu milioni 3 waliokuwa bila usalama wa chakula.

Wengine milioni 7 ambao hali hao ilikuwa nafuu kidogo huenda wakafikia viwango vya ukosefu wa usalama wa chakula kabisa, iwapo hali itaendelea kama ilivyo, OCHA imeongeza, ikitaja uchambuzi uliofanywa na shirika la chakula duniani, WFP.

Bazoum mwenye umri wa miaka 63 alizuiliwa Julai 26 na kundi la walinzi wake, yakiwa mapinduzi ya 5 tangu Niger kujipatia uhuru wake kutoka kwa Ufaransa hapo 1960. WFP imesema kwamba inaendelea kupeleka chakula kwenye taifa hilo la Sahel lisilo na bandari, licha ya hali ya kisiasa iliyopo.