Mwanaharakati aliyeko kifungoni Narges Mohammadi ashinda  tuzo ya Amani ya Nobeli

Mwanaharakati wa Iran Narges Mohammadi akionesha ishara ya ushindi

Mwanaharakati aliyeko kifungoni Narges Mohammadi alishinda Tuzo ya Amani ya Nobel siku ya Ijumaa kwa kupambana kwake na ukandamizaji wa wanawake nchini Iran.

Anapigania wanawake dhidi ya ubaguzi wa kimfumo na ukandamizaji, alisema Berit Reiss-Andersen, mwenyekiti wa Kamati ya Nobel ya Norway ambaye alitangaza tuzo hiyo huko Oslo.

Mamlaka ilimkamata Mohammadi mwezi Novemba baada ya kuhudhuria ukumbusho wa muathirika wa maandamano ya ghasia ya mwaka 2019. Mohammadi ana historia ndefu ya kifungo, hukumu kali na pia wito wa kimataifa umetolewa kwa ajili ya mapitio ya kesi yake.

Kabla ya kufungwa jela, Mohammadi alikuwa makamu wa rais wa Kituo kilichopigwa marufuku cha Watetezi wa Haki za Binadamu nchini Iran. Mohammadi amekuwa karibu na mshindi wa Tuzo ya Amani ya Nobel ya Iran Shirin Ebadi, ambaye alianzisha kituo hicho.