Matokeo ya uchaguzi Tanzania yaendelea kutolewa.

Watu wakiwa kwenye mstari wa kupiga kura.

Matokeo ya uchaguzi huo wa rais, bunge na udiwani yameendelea kutolewa kutoka maeneo kadhaa huku tume ya uchaguzi ikisema iko karibu kufikia asilimia hamsini ya matokeo hayo.

Baada ya kumalizika kwa shughuli ya kupiga kura kwenye uchaguzi mkuu nchini Tanzania, lililobaki sasa ni kujua matokeo ya uamuzi uliofanywa na wapiga kura.

Matokeo ya uchaguzi huo wa rais, bunge na udiwani yameendelea kutolewa kutoka maeneo kadhaa huku tume ya uchaguzi ikisema iko karibu kufikia asilimia hamsini ya matokeo hayo.

Mwandishi wetu wa Dar es salaam Dinaha Chahali amezungumza na VOA na kwanza Harrison Kamau alitaka kujua ikiwa matokeo ya uchaguzi yamefikia wapi.

Your browser doesn’t support HTML5

Matokeo ya uchaguzi Tanzania

Vile vile ametaka kujua kutoka kwake iwapo matokeo hayo yanapokelewa kwa njia ya amani. Hata hivyo ameeleza kuwa kumeripotiwa hali ya taharuki katika maeneo kadhaa