Afisa wa uchaguzi nchini Myanmar apigwa risasi akiwa ndani ya gari lake

Ramani ya Myanmar na vitongoji vyake

Sai Kyaw Thu naibu mkurugenzi mkuu wa Tume ya Uchaguzi ya Muungano iliyoteuliwa na jeshi alipigwa risasi mara kadhaa Jumamosi kulingana na ofisi ya habari wa jeshi, ripoti za vyombo vya habari, na taarifa ya uwajibikaji kutoka kwa kundi la msituni

Afisa wa ngazi ya juu wa uchaguzi nchini Myanmar alipigwa risasi akiwa ndani ya gari lake mjini Yangon ambao ni mji mkuu wa kibiashara wa nchi hiyo katika shambulio la hivi karibuni lililohusishwa na wanamgambo wanaoupinga utawala wa kijeshi.

Sai Kyaw Thu naibu mkurugenzi mkuu wa Tume ya Uchaguzi ya Muungano iliyoteuliwa na jeshi alipigwa risasi mara kadhaa Jumamosi kulingana na ofisi ya habari wa jeshi, ripoti za vyombo vya habari, na taarifa ya uwajibikaji kutoka kwa kundi la msituni.

Ofisi ya habari siku ya Jumapili ilisema shambulio hilo lilifanywa na People’s Defense Force kitengo chenye silaha kilichoundwa kinachoiunga mkono serikali ya umoja wa kitaifa inayounga mkono demokrasia, kundi la siri ambalo linaipinga serikali iliyowekwa na jeshi ambayo ilianzishwa wakati jeshi lilipochukua madaraka miaka miwili iliyopita.

Vikosi vingi vya upinzani vikiwemo vikundi vya Jeshi la Ulinzi la Wananchi vinafanya kazi kwa uhuru kutoka serikali ya umoja wa kitaifa lakini jeshi linawataja wote kama magaidi.