Alshabab wadai kuhusika na shambulizi Kenya.

Wanamgambo wa kundi la Alshabab lenye mahusiano na Alqaeda huko Somalia.

Kundi la wanamgambo wa kisomali la Alshabab limedai kuhusika na shambulizi kali la mpakani katika kituo cha Polisi cha Kenya ambalo liliuwa watu sita.

Shambulizi hilo lilitokea Jumamosi usiku katika kituo kimoja cha Polisi nje ya Damajelay karibu na mpaka wa Kenya na Somalia.

Afisa wa Kenya Adam Kaynan aliiambia idhaa ya Kisomali ya Sauti ya Amerika kwamba maafisa wa Polisi watatu walikuwa miongoni mwa waliouwawa na wengine wawili hawajulikani walipo.

Your browser doesn’t support HTML5

Mahojiano na Hussein Zuharuk.


Abdushakur Aboud amezungumza na mkazi wa kambi ya wakimbizi ya Dadaab karibu na mpaka wa Kenya na Somalia Bw.Hussein Zuharuk kuhusu mashambulizi hayo.