Upatikanaji viungo

Breaking News
Alhamisi, Februari 20, 2025 Local time: 10:39

UNDP: Kitovu kipya cha kimataifa cha itikadi kali za Kiislamu ni Afrika Kusini mwa Jangwa la Sahara


Viatu vya wanafunzi waliotekwa nyara kutoka Shule ya Sekondari ya Sayansi ya Serikali vinaonekana ndani ya chumba chao cha darasa Kankara, Nigeria, Jumatano, Desemba 16, 2020.
Viatu vya wanafunzi waliotekwa nyara kutoka Shule ya Sekondari ya Sayansi ya Serikali vinaonekana ndani ya chumba chao cha darasa Kankara, Nigeria, Jumatano, Desemba 16, 2020.

Kitovu kipya cha kimataifa cha itikadi kali za Kiislamu ni Afrika Kusini mwa Jangwa la Sahara ambako watu wanazidi kujiunga kwa sababu ya sababu za kiuchumi na kidogo kwa zile za kidini, inasema ripoti mpya ya shirika la maendeleo la kimataifa la Umoja wa Mataifa.

Ongezeko kubwa la asilimia 92 ya waajiri wapya kwa makundi yenye itikadi kali wanajiunga kwa ajili ya maisha bora ikilinganishwa na motisha ya wale waliohojiwa katika ripoti ya awali iliyotolewa mwaka 2017, kulingana na ripoti ya UNDP iliyotolewa Jumanne.

Kumekuwa na kupungua kwa asilimia 57 kwa idadi ya watu wanaojiunga na vikundi vya itikadi kali kwa sababu za kidini, ilisema.

Takriban watu 2,200 walihojiwa kwa ajili ya ripoti hiyo katika nchi nane za Afrika: Burkina Faso, Cameroon, Chad, Mali, Niger, Nigeria, Somalia, na Sudan.

Zaidi ya waliohojiwa 1,000 ni wanachama wa zamani wa vikundi vya itikadi kali, walioajiriwa kwa hiari na pia kulazimishwa, ilisema ripoti hiyo.

XS
SM
MD
LG