Upatikanaji viungo

Breaking News
Jumamosi, Septemba 28, 2024 Local time: 12:31

Timu ya Rugby ya Afrika Kusini yafanikiwa kutinga fainali ya kombe la dunia


Cheslin Kolbe wa Afrika Kusini akisherehekea kuifungia timu yake goli la pili wakati wa fainali ya Kombe la Dunia la Raga kwenye Uwanja wa Kimataifa wa Yokohama kati ya Uingereza na Afrika Kusini mjini Yokohama, Japan, Novemba 2, 2019.
Cheslin Kolbe wa Afrika Kusini akisherehekea kuifungia timu yake goli la pili wakati wa fainali ya Kombe la Dunia la Raga kwenye Uwanja wa Kimataifa wa Yokohama kati ya Uingereza na Afrika Kusini mjini Yokohama, Japan, Novemba 2, 2019.

Timu ya taifa ya Rugby ya Afrika Kusini imefanikiwa kuingia fainali ya michuano hiyo ya kombe la dunia baada ya kuishinda Uingereza kwa pointi 16-15 katika mchezo mkali na kusisimua ambao Uingereza walitawala kwa sehemu kubwa.

Timu ya taifa ya Rugby ya Afrika Kusini imefanikiwa kuingia fainali ya michuano hiyo ya kombe la dunia baada ya kuishinda Uingereza kwa pointi 16-15 katika mchezo mkali na kusisimua ambao Uingereza walitawala kwa sehemu kubwa.

Nahodha Siya Kolisi na kocha Jacques Nienaber walisema mabingwa hao watetezi walilazimika kutumia nguvu zao zote ili kupata ushindi wao finyu wakitokea nyuma katika uwanja wa Stade de France ili kujikatia tiketi ya kucheza fainali wikendi ijayo dhidi ya timu ya New Zealand.

Ilikuwa ngumu sana leo, lakini kazi ngumu tuliyofanya imezaa matunda na ndivyo mabingwa wanavyofanya," Kolisi alisema wakati wa kusherehekea ushinmdi mwishoni mwa mchezo huo.

Flyhalf Handre Pollard, ambaye aliingia kuchukua nafasi ya Mannie Libbok wakati Afrika Kusini ilipokuwa ikishambuliwa sana katika kipindi cha kwanza alipiga shuti la mbali na kuipatia ushini Springboks katika mechi hiyo.

Forum

XS
SM
MD
LG