Upatikanaji viungo

Breaking News
Alhamisi, Februari 20, 2025 Local time: 17:10

Rais wa zamani wa Ghana John Mahama apitishwa na Chama kikuu cha upinzani kuwa mgombea wake 2024


Rais wa zamani wa Ghana John Mahama alipitishwa na Chama kikuu cha upinzani nchini Ghana National Democratic Congress, kuwa mgombea wake mwaka 2024.
Rais wa zamani wa Ghana John Mahama alipitishwa na Chama kikuu cha upinzani nchini Ghana National Democratic Congress, kuwa mgombea wake mwaka 2024.

Chama kikuu cha upinzani nchini Ghana, National Democratic Congress, kilipiga kura kwa idadi kubwa  Jumamosi kumpitisha  rais wa zamani, John Mahama, kama mgombea  wake katika uchaguzi ujao  wa urais mwaka 2024.

Hii ni mara ya tatu kwa Mahama kuwania nafasi hiyo ya juu nchini Ghana, mojawapo ya nchi zenye demokrasia imara zaidi barani Afrika. Alishika nafasi ya pili nyuma ya Rais Nana Akufo-Addo mwaka 2016 na 2020.

Uchaguzi ujao wa urais unatarajiwa kuwa na ushindani mkali. Hakuna chama ambacho kimewahi kushinda zaidi ya mihula miwili mfululizo na nchi hiyo iko katika hali mzozo mbaya wa kiuchumi katika kizazi hiki, ambao umeongeza gharama ya maisha na kusababisha sarafu ya cedi kuporomoka, na hivyo kuchochea maandamano.

Mahama, mwenye umri wa miaka 64, alipata kura 297,603, ikiwa ni asilimia 98.9 ya kura zilizopigwa, tume ya uchaguzi ilisema mapema Jumapili.

XS
SM
MD
LG