Upatikanaji viungo

Breaking News
Jumanne, Machi 11, 2025 Local time: 14:20

Rais Felix Tshisekedi aapishwa kuongoza  muhula wa pili wa miaka mitano DRC


Rais wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo Felix Tshisekedi aliapishwa kuongoza  muhula wa pili wa miaka mitano Jumamosi Januari 20,2024. AP
Rais wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo Felix Tshisekedi aliapishwa kuongoza  muhula wa pili wa miaka mitano Jumamosi Januari 20,2024. AP

Rais wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo Felix Tshisekedi aliapishwa kuongoza  muhula wa pili wa miaka mitano Jumamosi baada ya ushindi wa kishindo ambao wapinzani wake wamekataa kuutambua kutokana na dosari zilizoenea katika uchaguzi mkuu wa mwezi Desemba.

Mamlaka imekiri kulikuwa na matatizo lakini wakatupilia mbali madai kuwa kura ziliibiwa. Mzozo huo uliozua tafrani unarudia mizozo ya awali ya uchaguzi ambayo ilichochea machafuko nchini Congo.

Tshisekedi alikula kiapo kwenye uwanja wa michezo katika mji mkuu Kinshasa uliokuwa umejaa wafuasi wakipeperusha bendera ndogo ndogo, maafisa wa serikali, wakuu wa nchi za Afrika na wajumbe wengine wa kigeni wakiwemo kutoka Marekani, China na Ufaransa.

Huku askari walio na silaha wakiwa wametapakaa kote katika mji mkuu, kulikuwa hakuna ishara ya mara moja kwamba wafuasi wa upinzani mjini Kinshasa walikuwa wakisikiliza wito kutoka kwa wapinzani wawili wakuu wa Tshisekedi kupinga kuchaguliwa kwake tena.

Forum

XS
SM
MD
LG