Upatikanaji viungo

Breaking News
Alhamisi, Septemba 19, 2024 Local time: 20:32

Marekani yatoa ombi la kujiunga tena na UNESCO


Nembo ya UNESCO kwenye makao makuu mjini Paris Ufaransa.
Nembo ya UNESCO kwenye makao makuu mjini Paris Ufaransa.

Mataifa wanachama wa UNESCO wanakutana baadaye wiki hii ili kujadili azma ya utawala wa rais wa Marekani Joe Biden ya kujiunga tena.

Hatua hiyo kwa shirika hilo la Umoja wa Mataifa lenye makao yake mjini Paris, hatua inayotarajiwa kuongeza mamilioni ya dola, pamoja na kuipa Marekani usemi kwenye program kadhaa kama vile mabadiliko ya hewa, elimu na intelijensia ya kubuni.

Wengi wanatarajia kwamba ombi hilo litakubalika wakati wa kikao maalum cha UNSECO kitakachofanyika Alhamisi na Ijumaa.Kufikia sasa hakujakuwa na pingamizi kutoka kwa mataifa yote 193 wanachama, ingawa China na Russia wametoa tahadhari kadhaa dhidi ya hatua hiyo.

Baadhi wanapendekeza kwamba Israel ambayo ilijiondoa kwenye shirika hilo inahitaji kufuata nyayo za Washington za kujiunga tena.

Forum

XS
SM
MD
LG