Upatikanaji viungo

Breaking News
Jumamosi, Septemba 28, 2024 Local time: 22:20

Marekani na Ufilipino wafanya doria ya pamoja ya kijeshi karibu na South China Sea


Ndege za kijeshi za Marekani na Ufilipino, karibu na South China Sea.
Ndege za kijeshi za Marekani na Ufilipino, karibu na South China Sea.

Marekani na Ufilipino wamekuwa wakifanya doria  ya pamoja ya anga na baharini huko  South China Sea, hatua ambayo inafanyika wakati nchi hizo mbili zikidisha ushirikiano, huku ukiwa na ongezeko la harakati za kichokozi za China katika eneo hilo.

Jeshi la anga la Ufilipino limesema Jumatano kwamba ndege yake ya kivita imeshiriki katika doria ya pamoja Jumanne, huko Batanes, ambalo ni jimbo la kaskazini mwa Ufilipino lililopo takriban kilomita 200 kutoka Taiwan, kisiwa kinachojitwala, ambacho China inadai kuwa himaya yake.

Zoezi hilo linaendelea hadi Alhamisi, likishirikisha wanajeshi wa majini wa Marekani na Ufilipino. Zoezi hilo limekuja siku chache tu baada ya rais wa Ufilipino Ferdinand Marcos Jr, kusema kwamba hali ni tete kwenye bahari hiyo, wakati China ikijaribu kusimika ushawishi wake, kwenye eneo hilo ambalo linazozaniwa na mataifa ya kieneo.

China imekuwa ikidai kumiliki maji yote ya South China Sea, suala ambalo limepelekea mzozo kati yake na Ufilipino, Vietnam, Malaysia, Taiwan na Brunei.

Forum

XS
SM
MD
LG