Upatikanaji viungo

Breaking News
Jumatano, Oktoba 23, 2024 Local time: 02:29
VOA Direct Packages

Jamaa za Rais wa zamani wa Niger zakanusha madai kuwa alijaribu kutorokea Nigeria


Rais wa Niger aliyeondolewa madarakani Mohamed Bazoum .
Rais wa Niger aliyeondolewa madarakani Mohamed Bazoum .

Jamaa za rais wa Niger aliyeondolewa madarakani Mohamed Bazoum wameambia shirika la habari la AFP Jumapili kwamba yupo salama, baada ya utawala wa kijeshi kudai alikuwa amejaribu kutoroka.

“Yupo kwenye makao ya Rais mjini Niamey akiwa na mke wake na mtoto wake wa kiume, na ameruhusiwa kupiga simu,” wanafamilia wameongeza. Taarifa zimeongeza kusema kwamba daktari wake aliruhusiwa kumuona, wakati akimpelekea chakula pia.

Utawala wa kijeshi uliomuondoa madarakani Julai 26 Alhamisi ulidai kwamba ulitibua jaribio la kuhepa la Bazoum kutoka alipozuiliwa. Msemaji wa utawala huo alisema kwamba Bazoum alipanga kujificha nje ya Niamey kabla ya kuondoka kwa helikopta ya kigeni, akielekea Nigeria.

Utawala huo umeongeza kusema kwamba baadhi ya wahusika wa mpango huo wamekamatwa. Wakili anayemuwakilisha Bazoum amekanusha madai hayo akisema kwamba ameendelea kuzuiliwa bila mawasiliano.

Forum

XS
SM
MD
LG