Upatikanaji viungo

Breaking News
Ijumaa, Oktoba 18, 2024 Local time: 15:26

China yaongeza vikwazo vya kiuchumi dhidi ya Taiwan kupinga matayarisho ya uchaguzi kisiwani humo


Wakazi wa Taiwan wakipeperusha vibendera vya taifa lao wakati wa siku kuu ya kitaifa Oktoba 1.,2023.
Wakazi wa Taiwan wakipeperusha vibendera vya taifa lao wakati wa siku kuu ya kitaifa Oktoba 1.,2023.

Serikali ya China Jumatano imetishia kuongeza vikwazo vya kibiashara kwa Taiwan, kama chama tawala kitaendelea na azma yake ya kuunga mkono uhuru, ikionekana kuendelea kwa vita vya  maneno, wakati uchaguzi wa kisiwa hicho ukipangwa kufanyika mwezi ujao.

Uchaguzi wa Taiwan wa rais na bunge wa Januari 13 unafanyika wakati ambapo China inakiona kisiwa hicho kuwa himaya yake, ikiilazimisha Taiwan kukubali madai ya china.

Taiwan mapema mwezi Desemba, iliishutumu China kwa kulazimisha kiuchumi na uingiliaji kati, baada ya Beijing kutangaza kuondoa ushuru kwenye baadhi ya bidhaa za kemikali zinazoagizwa kutoka kwenye kisiwa hicho, ikisema kuwa Taipei ilikiuka makubaliano ya kibiashara yaliyofikiwa mwaka 2010 kati ya pande hizo mbili.

Hilo limekuja baada ya China kusema imebaini kuwa Taiwan iliweka vikwazo vya kibiashara kinyume cha sheria za Shirika la Kimataifa la Biashara, WTO, na makubaliano ya wa biashara ya 2010.

Forum

XS
SM
MD
LG