Upatikanaji viungo

Breaking News
Jumanne, Septemba 17, 2024 Local time: 06:20

Papa Francis ameitembelea Papua New Guinea akisisitiza ulinzi wa rasilimali


Papa Francis akiwa Papua New Guinea
Papa Francis akiwa Papua New Guinea

Papa Francis aliwapongeza wenyeji wake kuwa matajiri katika utamaduni na rasilimali za asili ikiwemo dhahabu, shaba na mbao.

Papa Francis alitembelea Papua New Guinea leo Jumamosi, ambako alitoa wito kuhusu rasilimali nyingi za asili zinufaishe jamii nzima, katika shutuma za kisiasa zinazodaiwa katika nchi hiyo mahala ambako wengi wanaamini utajiri wao unaibiwa au kuvurugwa.

Akiwahutubia viongozi wa kisiasa na kibiashara, Papa huyo mwenye miaka 87 aliwapongeza wenyeji wake kuwa matajiri katika utamaduni na rasilimali za asili, ikiwa ni habari njema kwa akiba kubwa ya dhahabu, shaba, nikeli, gesi na mbao.

Lakini alipendekeza maelfu ya mabilioni ya dola yaliyopatikana kutokana na uchimbaji, usafishaji mafuta na uchimbaji wa gesi yalihitajika kunufaisha zaidi ya sehemu ya watu milioni 12 wa nchi hiyo.

Bidhaa hizi zimeletwa na Mungu kwa jamii nzima, Papa Francis alisema. Licha ya utajiri wake wa rasilimali, Papua New Guinea ni moja ya nchi maskini sana katika Pasifiki.

Forum

XS
SM
MD
LG