Upatikanaji viungo

Breaking News
Jumamosi, Mei 18, 2024 Local time: 08:02

OCHA kushirikiana na mashirika ya kibinadamu kukabiliana na manyanyaso ya kijinsia DRC


Mwathiriwa wa ubakaji akiwa amekaa nje ya kliniki ya Heal Africa huko Goma. Picha na AFP/Roberto SCHMIDT
Mwathiriwa wa ubakaji akiwa amekaa nje ya kliniki ya Heal Africa huko Goma. Picha na AFP/Roberto SCHMIDT

Shirika la Umoja wa Mataifa la misaada ya kibinadamu, OCHA, limesema kuwa linafanya kazi na mashirika mengine ya kibinadamu ili kusaidia kupunguza na kukabiliana na ongezeko la matukio ya unyanyasaji wa kijinsia huko Mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo.

Naibu mratibu wa misaada ya kibinadamu wa Umoja wa Mataifa kwa DRC, Suzanna Tkalec, alisema siku ya Jumatatu mjini Washington kuwa wanawake na wasichana katika majimbo ya Kivu Kaskazini, Kivu Kusini na Ituri wanaendelea kukabiliwa na viwango vya kutisha vya ukatili wa kijinsia kutokana na kuzuka upya kwa vurugu kati ya makundi ya wapiganaji na vikosi vya serikali.

Tkalec alisema ripoti ya hivi karibuni ya shirika la misaada la Madaktari Wasio na Mipaka iligundua kuwa wanawake na wasichana wapatao 90,000 walitafuta msaada wa matibabu baada ya kushambuliwa na kubakwa mwaka huu. Ripoti hiyo ilisema huenda waliojitokeza wanawasilisha sehemu ndogo tu ya jumla ya waathirika.

Tkalec anasema manusura hawana uwezo wa kuzifikia huduma za uokoaji maisha za unyanyasaji wa kijinsia au kuripoti unyanyasaji wao, wakihofia kunyanyapaliwa na jamii zao au wahalifu kulipiza kisasi.

"Mengi ya matukio haya ni ya kweli, kutokana na mazingira magumu wanayoishi wanawake na wasichana," Tkalec alisema.

Anasema OCHA haina uwezo mkubwa wa kutoa msaada kwa sababu mpango wake wa kukabiliana na masuala ya kibinadamu kwa mwaka 2023 unafadhiliwa kwa asilimia 38 tu.

Forum

XS
SM
MD
LG