Upatikanaji viungo

Breaking News
Jumamosi, Septemba 28, 2024 Local time: 02:14

Wanajeshi wa Korea Kaskazini waingia Korea Kusini kwa muda kabla ya kurejea


Picha kutoka wizara ya Ulinzi ya Korea Kaskazini ikionyesha wanajeshi wa Korea Kaskazini wakifanya kazi karibu na mpaka. Juni 18. 2024. ( AP)
Picha kutoka wizara ya Ulinzi ya Korea Kaskazini ikionyesha wanajeshi wa Korea Kaskazini wakifanya kazi karibu na mpaka. Juni 18. 2024. ( AP)

Korea Kusini imesema Jumanne kuwa darzeni ya wanajeshi wa Korea Kaskazini wamevuka mpaka  wenye ulinzi mkali, lakini wakarejea baada ya risasi za onyo kupigwa.

Hilo ni tukio la pili la aina hiyo ndani ya wiki mbili, wakati Pyongyang ikiendelea kuimarisha ulinzi wake kwenye mipaka yake na Kusini. Milipuko ya mabomu ya kutegwa ardhini karibu na mpaka huo pia imejeruhi wanajeshi kadhaa wa Korea Kaskazini, mkuu wa majeshi wa Kusini amesema, akiongezea kuwa Pyongyang hivi karibuni ilituma wanajeshi wake kwenye eneo hilo ili kufanya usafi, na kuweka mabomu ya ardhini, wakati uhusiano kati ya mataifa hayo mawili ukiendelea kudorora.

Mataifa hayo yamebaki katika hali ya vita baada ya mgogoro wa 1950- 1953 kumalizika, na kila mmoja kubaki akiwa amejihami, wakati eneo la mpaka lisilo na jeshi linaloigawa peninsula hiyo likisemekana kuwa na mabomu mengi ya kutegwa ardhini hapa duniani. Lakini Korea Kaskazini imeendelea kuimarisha uwekaji mabomu ya kutegwa ardhini, na kuimarisha mbinu za barabara na kuongezea kile ambacho kinaonekana kuwa vizuizi dhidi ya vifaru, jeshi la Seoul limesema.

Forum

XS
SM
MD
LG