Upatikanaji viungo

Breaking News
Ijumaa, Septemba 27, 2024 Local time: 16:29

Routh anafikishwa mahakamani kwa tuhuma za kutaka kumuua Donald Trump


Ryan Routh, mtuhumiwa wa jaribio la kutaka kumuua Donald Trump
Ryan Routh, mtuhumiwa wa jaribio la kutaka kumuua Donald Trump

Ryan Routh, mwenye miaka 58 ameshtakiwa kwa makosa mawili ya uhalifu wa bunduki. Bado hajajibu hoja hiyo.

Mtu anayetuhumiwa kujificha na bunduki karibu na uwanja wa gofu wa Donald Trump huko Florida katika jaribio la kumuua rais huyo wa zamani wa Marekani, anatarajiwa kufikishwa mahakamani leo Jumatatu, ambapo waendesha mashtaka watatoa hoja ya kutaka awekwe rumande hadi wakati wakesi yake.

Ryan Routh, mwenye miaka 58 ameshtakiwa kwa makosa mawili ya uhalifu wa bunduki, baada ya kudaiwa kuwa alielekeza bunduki kwenye mstari uliokuwa na mti hapo Septemba 15, wakati mgombea wa urais wa Republican alipokuwa akicheza gofu katika uwanja wake huko West Palm Beach, kulingana na makosa ya uhalifu. Bado hajajibu hoja hiyo.

Waendesha mashtaka wa Marekani wanaweza kutoa maelezo mapya kuhusu uchunguzi huo wakati wa usikilizwaji wa kesi hiyo, iliyopangwa kuanza saa tano asubuhi, huku wakidai kuwa Routh ni hatari kwa usalama wa umma, na lazima abaki chini ya ulinzi wakati akisubiri kesi yake.

Routh ameshtakiwa kwa kumiliki silaha wakati ambapo alikutwa ya uhalifu, na kumiliki silaha ambayo nambari yake ya siri ilifutwa. Mashtaka zaidi yanaweza kufuatia.

Forum

XS
SM
MD
LG